Ligi ya England timu 20 kushuka dimbani

Jumla ya timu 20 zinazoshiriki ligi ya England zinatarajiwa kushuka dimbani mwishoni mwa wiki.
Hata hivyo mechi ya Chelsea na Arsenal ,inaoonekana kuwa na mvuto zaidi kwa wengi, kufuatia matokeo ya mechi hiyo kutoa picha mbili tofauti, moja kuihakikishia Chealse ubingwa iwapo itashinda mechi hiyo,na pia Arsenal ikishinda italeta mazingira ya wazi kwa timu yoyote kati ya timu hizo mbili kutwaa ubingwa.
Naye kocha Liverpool Brendan Rodgers ameibuka na kutamba kuwa yeye ni kocha bora na hakuna kama yeye, huku akisema anamatumaini ya kuendelea kukinoa kikosi.
Pamoja na majigambo hayo Rodgers ameweka rekodi mpya ndani ya klabu hiyo kwa kuongoza misimu mitatu bila kuchukua taji lolote, tofauti na watangulizi wake tangu mwaka 1950.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao