Maelfu ya watu walala nje Nepal

Maelfu ya watu nchini Nepal wamelala nje usiku kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililoikumba nchi hiyo jana Jumamosi ambalo lilisababisha uharibifu mkubwa na kupotea kwa maisha.
Wakazi wa mji wa kathmandu walisema kuwa hawangerudi manyumbani mwao kutokana na hofu ya kutokea kwa mitetemeko zaidi.
Serikali ya Nepal inasema inaamini kuwa takriban watu 1500 wameaga dunia lakini idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka wakati makundi ya uokoaji yanapotafuta kwenye vifusi vya majengo yaliyoporomoka.
Hali mbaya ya hewa inalikumba eneo hilo na watoa huduma za dharura wanasema kuwa huenda ikavuruga jitihada za uokoaji.
Watu walala nje Nepal

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Shule ya msingi Nengo ya Walemavu, iliyoko wilayani Kibondo mkoani kigoma, inayohudumia wanafunzi walemavu wa mahitaji maalum inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni ukosefu wa maji Vifaa vya kujinfunza na kufundishia na vyombo vya kulia chakula