Nepal yasema inasimamia vyema misaada

Serikali ya Nepal imejitetea dhidi ya lalama kwamba inashindwa kusimamia vyema misaada ya dharura, kufuatia tetemeko kubwa la ardhi hapo Jumamosi.
Mkuu wa masuala ya dharura wa Nepal Rameshwor Dangal,ameambia BBC serikali inajitahidi iwezavyo, lakini mkasa huo ulikumba majimbo 20 nchini, na hivyo mahitaji ni mengi sana ndiposa serikali inalemewa.
Hali ya kutamauka imewakumba wengi waliothiriwa na tetemeko hilo,na wengine wameonesha malalamiko yao kwa kulumbana na polisi huko Kathmandu, mji mkuu wa taifa hilo.
Maelfu wameanza kuuhama mji huo mkuu.
Wanajeshi wakitoa misaada Nepal

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao