Changieni mfuko wa afya ya jamii mpate matibabu bora

Changieni mfuko wa afya ya jamii mpate matibabu bora


Taifa ili liweze kuwa na maendeleo lazima jamii iweze kujikinga na maradhi na  kuwa na afya bora na kuweza kuzalisha mali kwa ufasaha zaidi.

Kauli hiyo imetolewa na katibu tawala wilaya ya kibondo mkoa wa Kigoma Bw, Ayubu Sebabili wakati wa uzinduzi wa uhamasishaji wa uchangiaji wa mfuko wa afya ya jamii uliofanyika katika kijiji cha Bitare wilayani humo.

Sebabili amsema kuwa jamii lazima kuhakikisha inaelimishwa kuhusu uchangiaji wa mfuko wa afya jamii, ili iweze kuboreshewa na kupata matibabu kwa garama ndogo, ikilinganishwa na garama za matibabu zilivyo juu sana hivi sasa,  hali inayochangia kushuka kwa kiwango cha uchumi katika familia

  Nae meneja wa Bima ya Afya mkoa wa kigoma Bw, Odhiambo Eliasi amesema kuwa wananchi wakihamasishwa katika uchangiaji wa mfuko huo, changamoto zinazoukabili mfuko huo, zitakwisha maana madawa yatapatikana ya kutosha, kwa kuwa kiwango cha shilingi elfu 5 kwa kaya kwa mwaka ni kidogo ambacho mwananchi anaweza kukimudu

Mganga mkuu wa Wilaya ya Kibondo Laurian Kanegene amesema kuwa mfuko wa afya ya jamii wilayani humo, kwa mwaka huu umefaulu kununua dawa zenye thamani ya tsh million 44 mia 224 na 500 kutoka katika Boari kuu MSD kanda ya Tabora.

Amedai kuwa dawa hizo zitapelekwa katika zahanati zote nane na viuo vya afya viwili, vilivyoko wilayani humo na zitagawiwa kadri rekodi za makusanyo ya uchangiaji zilivyokwenda     

Hata hivyo baadhi ya wananchi waliokuwa katika mkutano huo ambao ni Joseph Bilaza na Vaileth Bulegea  wamesema kuwa ili mfuko huo uboreke vizuri pamoja na uhamasishaji unaoendela nilazima yafanyike kwa wachangiaji kama kupata dawa kama utaratibu unavyoeleza watumishi kutukia luga nzuri kwa wagonjwa.

Aidha wameeleza kuwa kumekuwepo na usumbufu kwa wagonjwa mara wanafika kwenye zahanati vituo vya afya na hospitali wakiambiwa kuwa dawa hazipo na kuelekezwa sehemu kwenda kununua hali ambayo imekuwa ikiwakatisha tamaa ya kujiunga na mfuko huo.kwani garama wanazotumia kununua madawa baada ya kuyakosa katika mfuko huo. zinazidi zile walizochangia 
Inserts wananchi

Baadhi ya watendaji katika sekta ya afya  wamesma kuwa wao wanakabiliwa na changamoto nyingi katika utendaji wao wa kazi, mmoja wa watendaji ambaye ni mganga wa zahanati ya Kijiji cha Bitare Bi, Rebeca John, amesema kuwa wanakabiliwa  changamoto mbalimbali  ikiwa ni pamoja na kuletewa dawa chache zisizokidhi mahitaji kwa watumiaji hali ambayo imekuwa ikisababisha malaumu kwa wagonjwa kuwa dawa hizo waganga  wanazitumia kwa matumizi yao binafis, pia kuuomba uongozi kuhakikisha unarekebisha hali hiyo ili mafanikio yawepo

Mwisho


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao