Wanafunzi wa shule ya msingi walalmikia kufanyishwa kazi za watu Binafsi mitaani na Walimu

fred eliasafu kaimu mkurugenzi Halimashauri W kibondo
Wanafunzi shule ya msingi Shunga
Joseph John mkuu wa shule ya msingi Shunga


Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Shunga iliyoko katika kijiji cha Kumuhama kata ya Bitare wilayani  kibondo mkoani kigoma wamelalamikia kitendo cha kufanyishwa kazi za watu binafsi kama kusomba matofari , kabeji na miwa kisha walimu kuchuka pesa baada ya wanafunzi kufanya kazi kwa  kwa madai kuwa ni za matumizi ya  shule

Baadhi ya wanafunzi hao wakiongea na na cliouds Tv kijijini hapo  wamesema kuwa wameporomoka kitaaruma kutokana na kufanyishwa kazi  za kubeba matofari ya wananchi , kabeji na miwa  kisha pesa kuchukuliwa na waalimu wa shule hiyo ambapo wamekuwa wakiambiwa kuwa zinaingia kwenye mfuko wa shule

Mkuu wa shule ya msingi shunga bw Joseph John nilimkuta shuleni hapo na alipoulizwa kuhusu swala hilo amekili wanafunzi kutumikishwa katika kazi hizo na kwamba waliamua kufanya hivyo ili kupata hela ya kumlipa mlinzi ili kulinda madawati mapya waliyoletewa na serikali na kwamba wazazi wamekuwa wakikaidi kuchangia pesa pale inapobidi

Baadhi ya wazazi waliopata kuzungumza na clouds katika kijiji cha kumuhama wamesema kuwa kitendo si kuzuri kwani wapo baadhi ya wanafunzi ambao afya zao haziridhishi hivyo ili zipo kazi ambazo hata wakiwa majumbani kwao uwa hawazifanyi na kutegeana na hali halisi ilivyo kwa mwanafunzi
Aidha wazazi hao wamesema kuwa  hawajashilirikishwa katika swala hilo lakini pamoja na hayo wamekuwa wakitoa mchango wao pale inapobidi  na kudai kuwa kama kuna tatizo katika swala la uendeshaji wa shule walimu husika wanatakiwa kupeleka katika uongozi wa serikali ya kijiji au kuitisha mkutano wa wazzi ili kujadili lakini mambo hayo hayafanyiki
Kwa upande  wake mratibu elimu  wa kata ya bitare Bi ISABERA NYUMAYINZU amesema kuwa wanaopaswa kuwajibika katika maswala ya kuwalipa walinzi na matumizi mengine ya shule ni wazazi kwa kushirikiana na uongozi wa kijiji na si wanafunzi
nae kaimu mkurugenzi wa halmashauru ya wilaya ya kibondo bw Fed Eliasafu amesema kuwa si utaratibu wanafunzi kufanyishwa kazi kwa watu binafsi na kwamba atalifanyia kazi na hatua sitahiki zitachukuliwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao