Kukwama kukamilika miradi ya maendeleo fedha za serikali kuchelewa

Kukwama kukamilika miradi ya maendeleo fedha za serikali kuchelewa


Halmashauri ya wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma inakabiliwa na changamoto ya kutokukamilika kwa miradi ya maenedeleo hususa ni katika miradi ya Maji Elimu na afya kwa sababu ya kuchelewa kwa wakati fedha za bajeti zinazokuwa zimetengwa na serikali  kuu

Hayo yamesemwa na Madiwani wakati wa kikao cha Baraza kilichofanyika wilayani humo,Madiwani hao, wamesema kuwa kuchelewa kufika  fedha hizo kumesababisha kutokukamilia kwa ujenzi wa miradi mbalimbali na kuwafanya wananchi wanaokuwa wamechangia nguvu zao kukata tamaa

Aidha wamesema kuwa katika bajeti ya mwaka 2014/2015 halmashauri hiyo ilidhinishiwa  kiasi cha shilingi billion 1.8 lakini hadi September 15 2014 fedha hizo zilikuwa bado hazijafika hali inayosababisha miradi mingi kubaki viporo huku wananchi wa maeneo husika wakikata tamaa  na kuto kuitikia kwa nguvu tena katika muendelezo wa miradi hiyo


Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Juma Maganga amesema kuwa kinachokwamisha miradi mingi ya maji iliyoko wilayani  kakonko inasimamiwa na halmashauri ya Kibondo kwakuwa hapo mwanzo ilikuwa wilaya moja na kugawanywa hivi karibuni  na kuwataka madiwani kutingiza mambo ya siasa kwenye maswala ya maendeleo kwakuwa kila kitu kiko wazi

 
Nao wananchi waliohudhulia kwenye Baraza hilo wamedai kuwa miradi mingi uwa inaelekezwa vijijini na washiriki wakubwa katika uchangiaji wa ujenzi huo ni wanavijiji nao wanakabiliwa na ukosefu kipato katika familia hivyo wanapojitoa na kisha kuona kile walichokuwa wanakiangaikia kinakwama ukata tama kabisa na kutotaka kushiriki wakati mwingine. 

Hata hivyo, wananchi hao wamesema hali hiyo usababisha kukosekana kwa huduma stahiki kama kukosa elimu bora Afya na Maji safi na kuleta usumbufu, na kuiomba serikali kuongeza raslimali fedha kwa wakati ili kuleta ufanisi na maendeleo yanayokuwa yamekusudi katika miradi husika



Mwisho
     

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao