Urais CCM kazi pevu

Dar es Salaam. 
Wakati joto la urais ndani ya CCM likiendelea kupamba moto, watu watakaoingia kundi la tano bora ambalo litapitishwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), wamefahamika.
Uchambuzi uliofanywa na makada mbalimbali wa chama hicho unaonyesha kuwa makundi hayo ambayo yatatoa wagombea mmoja, ni kundi la wagombea vijana, kundi la kifo, kundi la waziri mkuu aliyepo madarakani, wagombea wanawake na kundi la wagombea kutoka Zanzibar.
Kila kundi katika hayo litatoa mgombea mmoja ambaye jina lake litapelekwa kupitishwa kwenye mkutano wa NEC kupitishwa kabla ya kupigiwa kura kwenye Mkutano Mkuu wa CCM (CC).
Kundi la Vijana
Uchambuzi unaonyesha kwa vyovyote vile CCM lazima iteue jina la mgombea kijana hata kama watakuwa hawamtaki ili kuonyesha kuwa chama hicho kimekomaa na kinawapa moyo vijana kuwania nafasi za uongozi.
Wanasiasa vijana wa CCM ambao tayari wametangaza nia ya kuwania nafasi ya urais ni Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, January Makamba na Mbunge wa Nzega, Dk Hamis Kigwangalla.
Wengine ambao wamekuwa wakitajwa katika kundi hilo ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, Mbunge wa Songea Mjini, Dk Emmanuel Nchimbi, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja.
Kundi la vijana linatarajiwa kuwa na nguvu wakati wa mchakato huo, kutokana na kauli ya hivi karibuni ya Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM ambaye anaonekana dhahiri kulipigia chapuo.
Rais Kikwete akizungumza wakati wa maadhimisho ya Sikukuu ya Mwalimu Nyerere Oktoba 14 mwaka huu mjini Tabora, aliwataka vijana kumchagua mtu anayefanana na kijana kurithi nafasi yake.
Alirejea kauli hiyo alipokuwa akilihutubia taifa kupitia wazee wa Mkoa wa Dodoma Novemba 4, mwaka huu pale aliposema licha ya kauli yake ya awali kuwakera baadhi ya watu, lakini bado kuna umuhimu wa vijana kupewa nafasi za uongozi.
Kuna kundi lingine la wazi ambalo mgombea yeyote anaweza kulitumia kugombea kuwania nafasi hiyo ya uongozi wa juu wa nchi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao