Watanzania tulieni katika kipindi hiki cha mgawanyiko sababu Escrow

Mwemezi Muhingo Mwanachi

Watanzania wametakiwa kuwa watulivu katika kipindi hiki kinachoonekana kuwa  ni cha mapasuko katika Taifa kutokana na upotevu wa pesa ambazo ni mali ya umma toka katika account ya Esrow.

Hayo yalisemwa na kiongozi mmjoja wa Dini Mchungaji Eliasi Rugaganya wa Kanisa la kiinjili la Kirutheli Tanzania Dasisi Mashariki ya Ziwa Victoria Usharika wa Betherehem Nyakato Jijini Mwanza  wakati wa Ibada ya kipaimara iliyofanyika jana Jumapili kanisani hapo.

Rugaganya alisema kwakuwa katika nchi yetu ya Tanzania vipo vyombo ambavyo vinadhamana ya kuweza kushugulikia jambo hilo ni vema viachiwe kufanya kazi hiyo na wala wananchi wasijiingize katika migawanyiko inayoweza kusababisha  kuleta shida katia nchi

Aidha amevitaka vyombo vyote husika hasa vya kisheria kufanya kazi kwa umakini na uaminifu ili kurudisha Imani ya watanzania waliosambaratika kwa hivi sasa kutokana na kusikia kuwa pesa nyingi kama hizo zinachukuliwa na watu wachache tena bila utaratibu huku walio wengi wakikosa huduma za msingi katika miji na vijiji hususa ni kusuasua kwa kwa huduma za elimu Afya na maji.

Hata hivyo alisema kuwa kwa wale viongozi wa Dini  waliotajwa katika ripoti ya PAC hapo mwanzo kama  walifanya hivyo, na wakibainika watakuwa wameliaibisha Kanisa na kuvuruga Imani kwa wakristo wote hapa nchini Duniani kote kwani wao ni watu wanaotegemewa sana katika kulirejesha kanisa na wakristo wote katika uadilifu kwa kuyaacha maovu.

Alidai  kuwa hata kama pesa hizo  zilipitishwa kwao kwa ajili ya kufanya mambo frani ili wabaki na zingine bado  walifanya makosa kwani ni kinyume na maadili ya Mungu hivyo ni vyema kufuata taratibu na maadili ya Mungu ili hata wale wanaowafuata wawe waadilifu na baadae Taifa liwe na Amani na Watu wote waishi kwa amani na Furaha kaika nchi yao

Mwisho      .

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao