RC aipongeza Wilaya ya kibondo kwa mwendelezo wa ujenzi Maabara

                      KGOMA

RC aipongeza Wilaya ya kibondo kwa mwendelezo wa ujenzi Maabara

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Issa Machibya ameupongeza uongozi wa wilaya ya kibondo  na wananchi kwa ujumla juu ya kazi inayoendela katika mikoa na wilaya zote hapa nchini  ya ujenzi wa maabara katika shule za sekondari

Hayo ameyasema leo alipokuwa akiongea kikao cha dharula cha baraza la  Baraza Halmashauri wilaya ya kakonko mkoani kigoma katika kuhamasisha ujenzi wa maabara hizo,

Machibya amesema kuwa katika wilaya zote za mkoa huo ni wilaya mbili tu ambazo zina uhakika wa kukamilisha vizuri ujenzi huo mnamo November 30, 2014 ambazo ni Kigoma na Kibondo  huku akizitupia lawama zingine kuwa baadhi yao wamekuwa wakiwaachia wananchi peke yao kuwa waendelee na ujenzi na  wataalam kutokufanya kazi zao inavyostaili

‘’ Jambo hili halitakubalika kabisa nimekuta maeneo mengine wamejenga misingi ya tope kinyume na maelekezo alisema Machibya’’

Aidha ameeleza kushangazwa na kitendo cha wilaya ya kakonko kukutwa haijafanya maandalizi yoyote na kudai kuwa ni lazima ujenzi huo ukamilike muda uliopangwa kwani maendeleo haya ni kwa ajili ya watanzania wote hata kama serikali ndo ina hamasisha  na kuwataka viongozi wakaige mfano wilaya jirani ya kibondo ambapo wao waka kwenye hatua nzuri za ujenzi

Nae mkuu wa wilaya hiyo Piter Toyima amemuhakikishia kuwa muda uliopangwa ujenzi huo utakuwa umekamilika na kwa viwango vinavyotakiwa 


Machibya alianza ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo katika wilaya zote za mkoa wa kigoma ikiwa ni Kasulu, Kibondo Buhigwe Uvinza Kigoma vijijini na Kakonko.      

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao