MAAMBUKIZI YA VVU KIGOMA YAPANDA HADI ASILIMIA 3.4





Takwimu za maambukizi ya Virusi vya Ukimwi katika mkoa wa kigoma zinaonyesha kuwa  juu kwa asilimia 3.4 kwa utafiti wa mwaka 2011 na 2012 ikilinganishwa na utafiti wa 2007/2008 ambapo maambukizi yalikua asilimia 1.8 hali ilinayoonekana kusababishwa  muingiliano wa watu toka mikoa mbalimbali hapa nchini tofauti na miaka ya nyuma

Hali hiyo imetajwa kuwa utandawazi pamoja na kuiga mambo ya kisasa miongoni mwa baadhi ya jamii za mkoa huo imekuwa ni chanzo cha ongezeko la maambukizi ya virusi vya ukimwi kutokana na mabadiliko ya kimaendeleo na uelewa mdogo

Kama ilivyo kawaida  kutokana na mila na destuli za makabila mengi ya Tanzania, jamii na familia nyingi hapa nchini kuna mambo ambayo si lahisi wazazi kuwawekea wazi watoto wao kwa kuhofia uharibifu na kupelekea watoto kufikiri mambo makumbwa zaidi ya umri  hali ambayo inawapelekea kujiingiza katika vitendo vya kufanya mapenzi bila utaratibu na kabla ya wakati

Baadhi ya wakazi wa mamlaka ya mji mdogo wa kibondo mkoani hapo, wamesema kuwa yapo mambo mengi ikiwa ni umasikini ulevi wa pombe madawa ya kulevya kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya kijikinga na maambukizi katika makundi ya rika mbalimbali na wengine kufanya makusudi hatua ambayo wameitaja kuwa wamekuwepo wanaume ambao wamekuwa wakitumia uwezo wao wa kifedha kwa kuwarubuni watoto wadogo wa shule za msingi na sekondari, kufanya nao matendo ya ngono bila utaratibu   kwakuwa wengi wao kutegeana na umri  wao kuwa mdogo



Hayo yamejili baada ya baadhi ya wakina dada na wakina mama wilayani hapa kuamua kulalamika kuwa  wamekuwepo baadhi ya wanaume na vijana wa kiume kuamua  kuchana mipira ya kiume  Condom, mara msichana na mvulana au mwanaume kukubaliana kufanya mapenzi hali ambayo imekua ikiwanya waishi kwa hofu kuwa wameambukizwa

Tatua ielezwa katika kikao cha baraza la Madiwani cha Halmashauri ya wilaya hiyo ambapo madiwani walisema kuwa  imewalazimu wasichana kuiomba Idara ya Afya kupitia kitengo cha ukimwi kusambaza condom za kike ili wawe na uhuru wa kufanya mapenzi bila mashaka


Mratibu wa kitengo cha ukimwi wilaya ya kibondo Emmanuel Makunja alipoulizwa kulikono hadi jamii iombe mipira hiyo ya kike kwa ajili ya kujikinga na maambukizi wakati ilitakiwa iwepo sawa na mipira ya kiume amesema kuwa kulikukuwepo na tatizo la upatikanaji wa condom hizo lakini hivi sasa zimesha patikana na wanataraji kuanza kuzisambaza


Kwa upande wao baadhi ya vijana walipoulizwa na clouds, wamesema kuwa kinacho sababisha ni uelewa mdogo juu ya kijikinga na VVU kwa kuwa vijana wengi wanadai kuwa wakitumia mipira hiyo hawajisijii vizuri na, mtu anafanya hvyo ili yule mpenzi wake aweze kumkumbuka siku nyingine na wengine wanafanya hivyo makusudi, baada kujigundua kuwa wameshapata maambukizi



 Nao wakina Dada na wanawake wamedai kuwa mtu anayefanya kitendo kama hicho cha kuchana condom wakati wa kufanya mapenzi, huyo anakuwa anajua wazi hali ya afya yake kwa  kumuambikiza mwenzake na pia mabinti  wengi uelewa wao ni mdogo ikichangiwa  na  umasikini na Tamaa za vitu vidogo vidogo


Aidha wamesema  kuwa  mtu yeyote atakaye fanyiwa kitendo hicho asikae kimya ni vizuri afike kwenye vyombo vya sheria, na akapime afya ili kujiridhisha kama usalama kwa sababu hiyo ni aina ya unyanyapaa  na kuleta athali katika maisha ya watu


 Mwisho  



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao