mwanzo Ajali yaua 12 Morogoro

Morogoro. Watu 12 wamefariki dunia papohapo na wengine ambao idadi yao haijafahamika wamejeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria  kugonga treni ya abiria eneo la Kiberege, Ifakara Wilaya ya Kilombero.
Ajali hiyo iliyohusisha basi la Kampuni ya Aljabir ilitokea jana saa 9:15 alasiri.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo alisema miongoni mwa waliokufa katika ajali hiyo, sita ni wanaume, wanne wanawake na watoto wawili mmoja wa kike na mwingine wa kiume. Paulo aliwataja marehemu watatu waliotambulika kuwa ni Frugensia Lusangila (60) na Albeta Lusangila (62) wakazi wa Ichonde Tarafa ya Mang’ula na Joseph Kazwila (34) mkazi wa Dar es Salaam.
 Akielezea chanzo cha ajali hiyo Kamanda Paulo alisema, dereva wa basi hilo alivuka barabara yenye makutano na reli bila ya kuchukua tahadhari na kuigonga treni.
Alisema kuwa majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika Hospitali ya Mtakatifu Francis Ifakara na Kituo cha Afya Kibaoni kwa matibabu.
Alisema dereva wa basi hilo alikimbia mara baada ya ajali hiyo kutokea na polisi wanaendelea kumtafuta.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao