Serikali kuimarisha huduma za kifedha

SERIKALI imedhamiria kuimarisha upatikanaji wa huduma za fedha nchini, ili kufikia asilimia 50 ifikapo mwaka 2016.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa alisema hayo mjini Dodoma Juzi wakati wa uzinduzi wa huduma ya ‘Airtel Money Timiza’ yenye lengo la  kuwapatia mikopo wateja kwa kupitia simu zao za mkononi.
Alisema huduma ya ‘Airtel Money Timiza  inayoshirikiana na  kampuni ya Pan-African (AFB) ni mpya Afrika na duniani kote  ambapo itawasaidia wateja kupata mikopo ya muda mfupi.
Profesa Mbarawa alisema takwimu za Benki Kuu ya Tanzania (BoT) zinaonyesha hadi sasa kuna taasisi 52 zinazojihusiaha na utoaji wa huduma za kifedha,  hivyo kuchangia  upatikanaji mdogo wa huduma za kifedha.
 “…Takwimu rasmi zinaonyesha kuwa kati ya  mwaka 2013 na 2014 kulikuwa  watumiaji  wa simu wapatao 972,600,000  ambao hukamilisha miamala mbalimbali kwa  kutumia simu za mikononi kufanya manunuzi   yanayofikia  trilioni 28.3,” alisema.
Katika hatua nyingine, Profesa Mbarawa aliisifu kampuni ya Airtel kwa uvumbuzi wao ambao pia utachangia kasi ya ukuaji wa uchumi kwa njia ya mawasiliano.
Akizungumzia  huduma ya  ‘Airtel  Money Timiza’, Mkurugenzi Mtendaji  wa kampuni hiyo, Sunil Colaso alisema ili kupata huduma hiyo mteja hatatakiwa kuweka amana yeyote ile, lakini pia  mhusika atatakiwa kulipa mkopo wake kwa wakati  na kuseama kuwa kuna mkopo wa siku 7,14 na 28.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao