Migogoro ya wakulima na wafugaji nchini, chanzo ni ikiukwaji wa taratibu kwa viongozi

Mwemezi Muhingo Kibondo

Migogoro ya wakulima na wafugaji  inayoendelea katika maeneo mengi hapa nchini, inasababishwa baadhi ya viongozi kutokuwa elimu juu utambuzi wa migogoro hiyo, na wengine kuacha makusudi kwa kutofuata sheria na taratibu

Akitoa taarifa yake kamanda wa polisi wilaya ya kibondo mkoa wa kigoma SP Marko Joshua. wakati wa semina elekezi kwa ajili ya viongozi wa ngazi mbalimbali na wadau wa maendeleo, iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri kibondo amesema kuwa jamii kubwa imekuwa ikikosahaki zao za msingi kwa sababu ya baadhi ya viongozi wasiojua na kufuata sheria kwa kuwasababishia migogoro na kugombana wao kwa wao.

Joshua aliesema kuwa  wakulima na wafugaji wote wanastaili haki zao kwa mujibu wa sheria za Tanzania na hatua madhubuti hazitachukuliwa kutaingia mgogoro mkubwa ambao itakuwa vigumu kuudhibiti na kusababisha madhara makubwa katika jamii.

‘’Halmashauri nyingi hapa nchini hazijaona kuwa jukumu la kuhakikisha usalama katika jamii utulivu, na ulinzi wa mali za watu ni lao hivyo, kutotekeleza sheria namba 7 ya 1982 sheria ya serikali za mitaa  na badala yake jukumu hilo limeachiwa jeshi la polisi peke  alisema OCD Joshua’’

Hata hivyo alisema kuwa hivi sasa serikali kuu inaelekeza huduma mbalimbali za kijamii kwenda kwa wanannchi kupitia serikali za mitaa ili kuinua maisha yao hivyo, moja ya  majukumu ya viongozi waliochaguliwa na wananchi kuhakikisha  wanajua matatizo yao  mahitaji na kuyapatia ufumbuzi sahihi na ikibidi kuyawasilisha kwenye ngazi za vyombo husika.

Alitanabaisha kuwa katika maeneo ya vijijini viongozi wengi wamekuwa wakijiamulia mambo bila kuwashikisha wananchi hali ambayo imekuwa ikizusha mitafaluku mikubwa hasa pale wanapoona jambo linafanyika ambalo hawakuhusishwa na kwenda kuohoji ili kufahamu taratibu zilizotumika [Comflict managemen]

Aidha alisema kuwa wafugaji na wawekezaji wamekuwa wakikaribishwa vijijini bila utaratibu kwakuwa wananchi ndiyo wenye maamuzi kuwa huyu aje au asije katika mikutano  muu wa vijiji, na badala yake watendaji wamekuwa wakitumia mihutasali tu tena bila kuzishirikisha idara  na kamati zingine katika maeneo hayo ila wao uamua kufanya wanavyojua na matatizo yakiishaanza,uliomba jeshi la polisi  kwenda kutumia nguvu hali ambayo imekuwa ikilisababishia lawama jeshi hilo toka katika jamii na kulichukia kwasababu ya kutokuizuaia migogoro mapema.

 Aidha alishauri kuwa ni vizuri kutambua migogoro aina ya mgogoro, chanzo na kuzuia mapema  kabla haijawa mikubwa na kuleta madhara, kuwepo mipango mizuri ya matumizi bora ya ardhi, Sheria na taratibu zifuatwe, na kujua athari zake mapema.

Kwa upande wao baadhi ya washiriki ikiwa ni Bw, Baruani Gwimo, Mtendaji kata Busagala  na Moshi Kasase wa kijiji cha kumukugwa, walikili kuwa matatizo mengi yamekuwa yakisababishwa na baadhi ya viongozi lakini  kinachochangia ni elimu ndogo ya kujua na kutokutambua athari  na aina za migogoro. Kingine ni kukosa maadili ya utumishi.

       

            

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao