Senet Wataka Parestina itambuliwe

Baraza la Seneti la Ufaransa limepiga kura kuunga mkono azimio linaloitaka serikali ilitambue taifa la Palestina na kuhimiza mazungumzo yaanze haraka kati ya Israel na Palestina.
Azimio hilo lilopendekezwa na kutetewa na wafuasi wa chama cha kisoshialisti,walinzi wa mazingira na wale wa chama cha kikoministi cha Ufaransa na ambalo haliilazimishi serikali kulitekeleza,limepita chupu chupu kwa sauti 153 dhidi ya 146.Maseneta wa upande wa upinzani wa kihafidhina UMP na wale wa kiliberali hawakuunga mkono azimio hilo.Wizara ya mambo ya nchi za nje ya Israel imewashukuru waliolipinga azimio hilo ambalo serikali ya Israel inasema "linawapatia risala mbaya wapalestina."
Kwa maoni ya mwasisi wa azimio hilo,Gilbert Roger "kutambuliwa dola ya Palestina ni hatua ya mwanzo ya kuanzishwa uhusiano sawia kati ya Israel na Palestina na sharti pekee la kuanzishwa mazungumzo ya dhati."Amesisitiza Ufaransa inabidi iukumbushe ulimwengu kwamba ugonvi kati ya Israel na Palestina si vita vya kidini,bali ni ugonvi wa ardhi.
Upande wa upinzani wa kihafidhina nchini Ufaransa umekumbusha jukumu la serikali katika kuhimiza mazungumzo ya amani.Seneta Christian Cambon wa chama cha UMP amesema na hapa tunukuu"Wapalestina wanastahili hali bora zaidi kuliko kutambuliwa karatasini.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao