Lord Coe kuwania Urais IAAF

Sebastian Coe ametangaza kuwania Urais katika shirkisho la riadha la International Association of Athletics Federations (IAAF) hapo mwakani.
Mshindi wa Olimpik mita 1500 mara mbili, kwa sasa ni makamu wa Rais wa shirikisho hilo tangu mwaka 2007.
Kwa kuongoza kikosi chake katika mashindano ya London mwaka 2012,Coe ametambulika zaidi na kuwa miongoni mwa wagombea wenye nguvu.
Lord Coe kwa sasa ametangaza waziwazi kutaka kuwania Urais wa shirikisho hilo huku akionekana kuimarika zaidi katika ushindani wa nafasi hiyo ya uongozi.
Mwanariadha huyu mwenye miaka 58 amewahi kuwa mshindi wa mbio ndefu ambapo alijipatia medali ya dhahabu mwaka 1980 na 1984.
Kipaumbele chake ni kuonyesha umhimu na uendelevu wa mchezo wa riadha kote duniani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao