Uingereza kuweka jeshi lake Bahrain

Uingereza imesaini makubaliano na Bahrain ya kujenga kituo cha jeshi la wanamaji nchini humo ambacho kitakuwa ndicho kituo cha kwanza cha jeshi la Uingereza eneo la mashariki ya kati tangu iondoke eneo hilo mwaka 1971.
Makubaliano hayo yaliafikiwa baada ya mieizi kadhaa ya mazungumzo.
Waziri wa ulinzi nchini Uingereza Michael Fallon alisema kuwa kituo hicho kitaliwezesa jeshi la wanamaji la Uingereza kuleta udhabiti eneo la Ghuba.
Mwandishi wa masuala ya usalama wa BBC anasema kuwa makubaliano hayo yanafanyika wakati nchi za Ghuba zinakabiliwa na tishio kutoka kwa wanamgambo wa Islamic State.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao