Uchaguzi Namibia mfano wa kuigwa Afrika

Chama cha Ukombozi wa Namibia SWAPO, kimeshinda kwa zaidi ya asilimia 86 ya kura za uchaguzi wa Rais wa nchi hiyo. Waziri Mkuu wa sasa Hage Geingob ndiye amechaguliwa kuwa Rais mpya, huku chama hicho ambacho kimekuwa madarakani tangu uhuru wa nchi hiyo mwaka 1990, kikiwa kimeshinda viti vingi vya kura za ubunge.
Uchaguzi huo umeelezwa kufanyika kwa ufanisi kwa kutumia vifaa vya kielektroniki.
Ili kufahamu undani wa hali ya mambo ilivyokuwa, nilizungumza na mkazi wa mji mkuu wa Namibia Windhoek bwana Mussa Nahimana ambaye ni Mrundi mwenye kufanya shughuli zake nchini humo. Kwanza nilimuuliza, uchaguzi huo ulifanyika kwenye mazingira gani kwa kuzingatia masuala ya utulivu na usalama?
Hata hivyo uchaguzi huo umekuwa tofauti na baadhi ya chaguzi nyingine za Afrika ambapo mivutano na kususia matokeo ni baadhi ya mambo ambayo hujitokeza, lakini Namibia walioshindwa na walioshinda wamekuwa katika sherehe ya pamoja.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao