Watu 7 wafariki katika milipuko Somalia

Takriban watu saba wamefariki katika milipuko miwili ya kujitolea muhanga katika mji wa Baidoa kusini mwa Somali.
Shambulizi hilo ambalo pia liliwajeruhiwa zaidi ya watu 20 lilitokea nje ya mgahawa unaopendwa sana na wakaazi na wanahabari.
Wawili ya waliofariki ni waandishi wa habari wanaofanya kazi na runinga za Somali kulingana na BBC Somali.
Makundi kadhaa ya wanamgambo yamekuwa yakipigania udhibiti wa Somali tangu rais Siad Barre ang'atuliwe Mamlakani mwaka 1991.
Nahodha Hassan Nor ameliambia shiriki la habari la AP kwamba mlipuaji wa kujitolea muhanga aliliendesha gari lake katikati ya kundi la watu na kujilipua.
Mlipuko wa pili ulitokea baada ya mlipuaji mwengine wa kujitolea muhanga kujilipua ndani ya mgahawa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao