Netanyahu atimua mawaziri wawili Israel

Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ameiweka nchi katika hali ya kufanyika mapema uchaguzi wa bunge kwa kuwafukuza kazi mawaziri wawili waandamizi ambao ni viongozi wa vyama katika serikali yake ya mseto. Wakati wa mkutano na waandishi wa habari kupitia televisheni, Bwana Netayahu amewashutumu mawaziri wote wawili akiwemo waziri wa Fedha, Yair Lapid, na waziri wa Sheria, Tzipi Livni, kwa kupanga njama dhidi yake.

Tzipi Livni Msuluhishi Mkuu wa Israel na Waziri wa Sheria aliyefukuzwa kazi

Bwana Netanyahu amesema amechukua hatua hiyo kwa kuzingatia madhara yanayoweza kusababishwa na kitendo hicho."Katika neno moja yanaitwa maasi, na hayo yanafanya isiwezekane kuendesha serikali, iwe vigumu kuongoza nchi, kwa hiyo muda mfupi uliopita nilimwagiza katibu wa baraza la mawaziri kutoa barua za kuwafukuza kazi mawaziri Livni na Lapid. Pia kutokana na ulazima wa kuhakikisha kunakuwepo serikali imara na yenye kufuata maadili, nimeamua kusukuma mbele sheria ya kuvunja bunge na kwenda katika uchaguzi haraka iwezekanavyo." amesema waziri mkuu Netanyahu.
Wanasiasa wote wawili viongozi wa vyama vya mrengo wa kati, wamesema nchi imetumbukizwa katika uchaguzi usio wa lazima. Mwandishi wa BBC nchini Israel amesema Bwana Netanyahu huenda akataka utawala mpya utakaovihusisha vyama vya dini vinavyowakilisha madhehebu ya Wayahudi wa ultra-orthodox.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao