Polis FC Kibondo, kidedea dhidi ya Agent FC kwa mabao 2 - .0



Michezo

Ligi ya Taifa Daraja la nne ngazi ya wilaya ilifikia tamati jana kibondo mkoani kigoma kwa kuzihusisha timu mbili za Polisi Fc na Ajent Fc amazo ndo zilifunga pazia hilo huku polisi Fc wakitoka kwa ushindi wa mawili  na Ajent Fc hawakupata kitu

Wakati wa sakata hilo, polisi walipata bao la kwanza katika dakika ya 18 amabalo liliingizwa kimyani na Katusi Manumbu na goli hilo lilidumu mpaka dakika ya 45 za kipindi cha kwanza

Katika hali iliyowashtua mashabiki wa timu ya Agent  katika dakika ya 60 kipindi cha pili mchezaji wa timu hiyo, Bw, Jelison Moshi,  aliipatia timu ya polis FC, bao la pili kwa kujinga mwenyewe ambapo mabao hayo yalidumu hadi dakika 90 za mchezo

Timu zilizoshiriki Ligi hiyo ngazi ya wilaya ni Mbwamwitu FC, walioondoka na kombe  kwakuwa mshindi wa kwanza kwa kupata point 7, Polis FC alipata point 6, Kibondo young stars waaliapata point 3 huku mshindi wa nne akiwa ni Ajent FC point 1 

Kwa mujibu wa Katibu chama cha mpira wa miguu Wilaya ya kibondo Bw, James Samson  wakati wakizungumza na Gazeti hili alisema kuwa  matokeo ya mwaka huu  hayana tofauti na mwaka jana  na kuwataka  wachezaji wa timu zote kujikita zaidi katika mazoezi ili  kuboresha na kuinua viwango vya uchezaji

Aidha Samsoni alisema kuwa hivi karibuni wanatarajia kwenda mjini kigoma ili kushiriki Ligi ya mkoa ambapo mshindi wanza aliyechukua kikombe atapewa kipaumbele, pia amewataka wadau mbalimbali wa michezo kuendelea kujitokeza kuwaunga mkono wanamichezo wote ndani ya wilaya ya kibondo mkoani kigoma.

Hata hivyo mmoja  wa washiriki wa mchezo wa mpira wa miguu Bw, Katusi Manumbu ambaye ni mchezaji wa timu ya polis Fc alieleza changamoto wanazokabiliana nazo pamoja na ukosefu wa viwanja vizuri vya kufanyia mazoezi  na michezo kwa ujumla kwani hata uwanja unaotegemewa hapa wilayani ni kokoto  tupu hali ambayo imekuwa ikiwakatisha tama wachezaji wengi wakihofia kuumia


Katusi alitanabaisha kuwa timu nyingi zinakosa vifaa vya michezo hata ushikishwaji mdogo tofauti na maeneo mengi katika mikoa mingine hapa nchini, alisistiza kuwa katika mkoa huu wa kigoma kuna watu wenye vipaji vizuri vya michezo hasa kabumbu wameachwa nawo wanakosa hata pa kuanzia

Mwisho 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao