Mswada wa ugaidi Kenya wawakera wengi

Bunge la Kenya limepitisha mswada unaolenga kuwapa nguvu zaidi maafisa usalama kukabiliana na ugaidi pamoja na maswla mengine ya usalama.
Wabunge walihusika na mjadala mkali Alhamisi kabla ya mswada huo kupitishwa huku upinzani ukisema kuwa ikiwa itakuwa sheria itakuwa inakiuka haki za wananchi.
Wabunge hao pamoja na mashirika mengine ya kutetea haki za binadamu yanasema kuwa watafanya maandamani ikiwa mswada huo utapitishwa bila ya kufanyiwa mabadiliko ili isikiuke haki za binadamu.
Kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Al shabaab limekua likishambulia Kenya mara kwa mara wataalamu wa wakisema kuwa Kenya haina mikakati mizuri ya kudhibiti usalama wake.
Sheria hizo mpya zinampa Rais na mashirika ya ujasusi mamlaka mapya.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao