Mugabe awashtumu wapinzani wake chamani

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amelaumu watu fulani ndani ya chama tawala cha ZANU-PF kwamba wanapanga kumng'atua mamlakani.
Akihutubia kikao cha chama hicho, Mugabe amesema kuwa kuna majaribio ya kuwahonga wajumbe kumpinga kama kiongozi, lakini wajumbe hawawezi kupokea hongo.
Pia amemlaumu aliyekuwa naibu wake Joice Mujuru anayedaiwa kupanga kumng'atua na kumuita mwizi.
Chama tawala cha Zimbabwe kinakumbwa na vita vya ndani kwa ndani kuhusu ni nani atakayerithi nafasi ya Mugabe ambaye ana miaka 91 na ameilongoza taifa hilo tangu lijinyakulie uhuru.
Vilveile kiongozi huyo ametupilia mbali dhana ya kujiuzulu akisema ni upuzi .

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao