Jenerali aliyempinga Museveni arudi UG

Mwanajeshi wa Uganda ambaye alitofautiana hadharani na rais wa nchi hiyo Yoweri Museveni mwaka uliopita amerejea nchini Uganda bila kutarajiwa kutoka nchini Uingereza ambapo alikuwa amekimbilia uhamishoni.
Jenerali David Sejusa aliitoroka Uganda baada ya kumshutumu rais Museveni kwa kujaribu kubuni familia ya kifalme akitaka kumkabidhi uongozi mwanawe wa kiume.
Sejusa pia alidai kuwa kulikuwa na njama ya kuwaua watu fulani katika serikali na jeshini ambao walikuwa wakipinga mpango huo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao