Mambomu manane yaokotwa Kigoma

Mambomu manane yaokotwa Kigoma

Watu wawili waliokuwa wikichimba kifusi katika nyumba iliyokuwa ya diwani wa kata ya mabamba kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya waganga ya kituo cha afya mabamba wilaya ya kibondo mkoa wa kigoma. waliokota mabomu nane yanayosadikiwa kuwa yalifukiwa ardhini kwa zaidi ya miaka 10 katika eneo hilo

Mmoja wa wananchi hao waliokuwa wakichimba na kusogeza kifusi cha udongo  ikiwa ni mwendelezo wa ujenzi wa nyumba ya mganga katika kituo cha afya mabamba Bw fotunatus katabalo amesema kuwa yeye na mwenzake waliona vitu kama vyuma ambavyo walivitilia mashaka na  kumjulisha msimamizi wa ujenzi ambaye nae alichukua jukumu la kutaarifu uongozi wa kata  na mkuu wa kituo cha polisi mabamba kwa ajili ya utambuzi wa vitu hivyo kwani tayari baadhi ya watu walioviona walikwisha tambua kuwa ni mabomu

Msimamizi wa ujenzi wa nyumba hiyo ya mganga katika kituo cha afya mabamba bw flansisi petro alisema kuwa yeye alitaarifiwa na watu waliokuwa wakifanya kazi ya uchimbaji wa msinngi kwa ajili ya ujenzi ndipo naye aliamua kutaarifu uongozi wa kata kasha kutaarifu polis

Pamoja ni kwamba mabomu si kitu cha kukimbiia lakini mamia ya watu walifika kujionea tukio hilo na haya ndio yalikuwa maoni yao

Kwa mujibu wa mtaalamu wa mabomu kutoka kambi ya jeshi iliyoko kata ya kizazi bw damas Nyitambe amesema kuwa mabomu hayo huenda yamewekwa kadtika eneo hilo kwa zaidi ya miaka 10 kwa kuwa yameonekana kuwa na kutu na kwamba kama moja lingelipuka basi yote yangeweza kulipuka na kusababisha madhara makubwa na hapa anatoa elimu kwa mamia ya watu waliofika kujionea mabomu hayo bila kujali kuwa ni hatari kwa maisha yao

Kwa upende wake mwenyekiti wa ulinzi na usalama wilayani kibondo bw Venance mwamoto baada ya mamia ya watu kukfika mahali hapo ili kuona mabomu hayo amewataka wananchi kuwa makini na kutopenda kushangaa vitu vya hatari kama hivyo kwani yangeweza kulipuka na kusababisha maafa makubwa kutokana na umati mkubwa uliofika kushangaa

Ni mara nyingi kumekuwepo na upatikanaji wa mabomu katika maeneo mengi ya wilaya za kaonko na kibondo na mkoa mzima wa kigoma hali inayosadikiwa kuwa uenda yaliachwa na wakimbizi wan chi za Burundi Kongo Na Rwanda walioingia hapa nchini wakikimbia mapigano katika nchi zao

Kwakuwa wilaya hizo zinapakana  na nchi hizo na walikuwa wakiishi katika baadhi ya vijiji vya wilaya hizo


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao